• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
Oricho amepania kurejea kuchezea klabu za Ligi Kuu ya FKF-PL

Oricho amepania kurejea kuchezea klabu za Ligi Kuu ya FKF-PL

NA JOHN KIMWERE

KIUNGO wa zamani wa Chemelil Sugar, William Oricho anataka kurejea kushiriki kampeni za Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF-PL).

Mchana nyavu huyu ambaye husakatia Gogo Boys ya Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza anasema ingawa hawajamaliza kampeni za msimu huu klabu kadhaa za Ligi Kuu zinasaka sajili yake.

Kwenye klabu ya Chemelil Sugar alikuwa kati ya wachezaji wazuri kabla ya kukumbwa na matatizo ya kufedha hali iliyochangia kutofanya vizuri na kushushwa ngazi.

Kipindi hicho alikuwa karibu ajiunga na Wazito FC.

“Nataka kurejea kuchezea klabu za soka la ligi za juu msimu ujao maana tayari kuna timu zinazoulizia huduma zangu,” amesema na kuongeza kuwa kila mchezaji huwa anahitaji mafanikio.

Oricho aliyewahi kuchezea Vihiga United ana mkataba wa mwaka mmoja na Gogo Boys inayoshiriki kipute hicho kwa mara ya kwanza.

Anasema alipojiunga na klabu hiyo alipania kuisaida kupandishwa ngazi kushiriki kipute cha Supa Ligi ya Taifa (NSL) lakini anaona ni kama ndoto yao haitatimia.

Hata hivyo anshikilia kuwa amepania kuisaidia kuhakikisha wameshinda zote nne zimesalia.

Kwenye mechi zilizosalia, Gogo Boys itachuana na viongozi wa kipute hicho Dimba Patriots, kumenyana na Liberty FC, kupepetana na Ruiru Hotstars kisha kukutanishwa na Nairobi United.

  • Tags

You can share this post!

Balala abururwa hadi kortini kwa madai ya ufisadi

Joho aanza kumpigia Nassir debe

T L