• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Pigo kwa kipa Alisson Becker wa Liverpool baada ya baba mzazi kufa maji nchini Brazil

Pigo kwa kipa Alisson Becker wa Liverpool baada ya baba mzazi kufa maji nchini Brazil

Na MASHIRIKA

JOSE Agostinho ambaye ni baba yake kipa chaguo la kwanza la Liverpool, Alisson Becker, ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 57.

Kwa mujibu wa maafisa wa polisi waliohojiwa na vyombo vya habari nchini Brazil, inaaminika kwamba Agostinho alikufa maji katika mojawapo ya mabwawa lililokuwa karibu na nyumbani kwake.

Jose alikuwa ameenda kupiga mbizi katika bwawa moja katika mji wa Lavras do Sul, Brazil Kusini.

Baada ya kutoweka kwake kuripotiwa katika kituo cha polisi mnamo Jumanne ya Februari 23, rafiki yake mmoja na mfanyakazi wa nyumbani waliupata mwili wa Jose bwawani mnamo Jumatano usiku.

Sawa na wanawe wawili wa kiume, Alisson, 28, wa Liverpool na Muriel, 34, wa Fluminsense, Jose pia alikuwa kipa katika enzi zake za usogora.

Katika ya vikosi ambavyo vimemwomboleza Jose ni Fluminense, Sao Paulo, Chapecoense, Inter Milan,

Alisson alisajiliwa na Liverpool mnamo 2018 baada ya kuagana rasmi na kikosi cha AS Roma nchini Italia.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Dkt Ahmed Kalebi awapa motisha Gogo Boys kujitahidi zaidi...

Tarehe ya refarenda kujulikana mwezi Machi