Na MASHIRIKA
FOWADI Tyler Roberts sasa hatachezea waajiri wake Leeds United mchuano wowote msimu huu baada ya kufanyiwa upasuaji kwenye paja.
Nyota huyo raia wa Wales mwenye umri wa miaka 23 alipata jeraha baya akichezea waajiri wake dhidi ya Leicester City katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) mnamo Machi 5, 2022.
Kwa mujibu wa Leeds, Roberts atasalia mkekani kwa kipindi cha miezi mitatu ijayo.
Hivyo, atakosa kampeni muhimu za Leeds wanaojitahidi kukwepa shoka la kushuka ngazi katika EPL msimu huu na mchujo wa kwanza wa kuingia Kombe la Dunia dhidi ya Austria mwishoni mwa Machi 2022.
Kuongezea, Afisa Mkuu Mtendaji wa Shirikisho la Soka la Wales, Noel Mooney, amesema mechi kati yao na Ukraine nayo isingeahirishwa hadi Juni kama ilivyoombwa na Ukraine kutokana na vita kati yao na Urusi.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO