• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 2:31 PM
Poland wazamisha Andorra kirahisi katika gozi la Kundi I

Poland wazamisha Andorra kirahisi katika gozi la Kundi I

Na MASHIRIKA

SOGORA Matty Cash wa Aston Villa aliwajibishwa na timu ya taifa ya Poland kwa mara ya kwanza katika mchuano kufuzu kwa Kombe la Dunia 2022 ulioshuhudia Robert Lewandowski akifunga mabao mawili na hivyo kupepeta Andorra 4-1.

Ushindi huo uliwaweka Uingereza katika ulazima wa kusubiri hadi Novemba 15, 2021 watakapomenyana na San Marino ili kujikatia tiketi ya kuelekea Qatar mwaka ujao. Andorra walikamilisha mechi dhidi ya Poland wakiwa na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya Ricard Fernandez kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya sekunde 20 pekee za kipindi cha kwanza kwa kosa la kumpiga kumbo Kamil Glik.

Arkadiusz Milik alifunga bao la tatu la Poland mwishoni mwa kipindi cha kwanza kabla ya Lewandowski aliyefungua ukurasa wa mabao katika dakika ya tano kucheka na nyavu kwa mara nyingine kunako dakika ya 73. Kombora kutoka kwa Kamil Jozwiak lilifanya mambo kuwa 2-0 kabla ya Joan Cervos kuwarejesha Andorra mchezoni.

Cash aliyepata uraia wa Poland mnamo Oktoba 2021, aliletwa uwanjani katika dakika ya 64. Ushindi wa Poland watakaomenyana na Hungary katika mechi ya mwisho mnamo Novemba 15, uliwapaisha hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Kundi I kwa alama 20, tatu nyuma ya Uingereza.

Uingereza watakuwa wageni wa San Marino wakihitaji sare ya aina yoyote ili kujikatia tiketi ya kunogesha fainali za zijazo za Kombe la Dunia nchini Qatar.

You can share this post!

Kane afunga mabao matatu na kuongoza Uingereza kuponda...

Northern Ireland wasubiri Italia kwa hamu baada ya kukomoa...

T L