Na MASHIRIKA
PARIS Saint-Germain (PSG) walianza kampeni zao za Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) katika msimu wa 2021-22 kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya limbukeni Troyes.
Mabao ya PSG yalifumwa kimiani kupitia Achraf Hakimi na Mauro Icardi baada ya Oualid El Hajjam kuweka Troyes uongozini.
Kati ya sajili wapya wa PSG, ni kiungo wa zamani wa Liverpool, Georginio Wijnaldum ndiye wa pekee aliyewajibishwa katika mchuano huo uliokosa maarifa ya kipa Gianluigi Donnarumma na beki Sergio Ramos.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO