• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 11:53 AM
PSG waanza msimu mpya wa Ligue 1 kwa kupepeta limbukeni Troyes

PSG waanza msimu mpya wa Ligue 1 kwa kupepeta limbukeni Troyes

Na MASHIRIKA

PARIS Saint-Germain (PSG) walianza kampeni zao za Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) katika msimu wa 2021-22 kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya limbukeni Troyes.

Mabao ya PSG yalifumwa kimiani kupitia Achraf Hakimi na Mauro Icardi baada ya Oualid El Hajjam kuweka Troyes uongozini.

Kati ya sajili wapya wa PSG, ni kiungo wa zamani wa Liverpool, Georginio Wijnaldum ndiye wa pekee aliyewajibishwa katika mchuano huo uliokosa maarifa ya kipa Gianluigi Donnarumma na beki Sergio Ramos.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Haaland afungia Dortmund mabao matatu katika German Cup

Wanatenisi wa Kenya watua nchini Misri kwa mashindano ya...