Na MASHIRIKA
CHIPUKIZI Erling Braut Haaland, 21, alifunga mabao matatu chini ya dakika 25 na kusaidia Borussia Dortmund kupepeta Wehen Wiesbaden 3-0 katika kivumbi cha German Cup.
Haaland ambaye ni raia wa Norway, amekuwa akiwaniwa pakubwa na Chelsea baada ya kufungia Dortmund mabao 27 katika Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) mnamo 2020-21.
Chini ya kocha Marco Rose, Dortmund watakuwa wenyeji wa Eintracht Frankfurt katika mechi ya kwanza ya Bundesliga muhula huu mnamo Jumamosi ya Agosti 14, 2021.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO