• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 9:50 AM
Quins na Monks waonja ushindi wa kwanza Ligi Kuu ya raga Kenya Cup ikienda likizo ya Krismasi

Quins na Monks waonja ushindi wa kwanza Ligi Kuu ya raga Kenya Cup ikienda likizo ya Krismasi

Na GEOFFREY ANENE

KENYA Harlequin na Monks ya Chuo Kikuu cha Kikatoliki wameandikisha ushindi wao wa kwanza kwenye Ligi Kuu ya raga nchini (Kenya Cup), Jumamosi.

Quins walikung’uta Mean Machine ya Chuo Kikuu cha Nairobi 45-20 uwanjani RFUEA nao Monks wakaduwaza mabingwa wa zamani Mwamba 24-23 katika Chuo Kikuu cha Strathmore.

Wanabenki wa KCB walidumisha uongozi wao kwenye ligi hiyo ya klabu 12 walipopepeta Nakuru 45-10 uwanjani Nakuru Athletic. KCB, ambao walipata pointi zao kupitia kwa Michael Kimwele (miguso miwili), Elvis Olukusi, Brian Wahinya, Samuel Asati (mguso mmoja kila mmoja) na Darwin Mukidza (mikwaju miwili).

Mabingwa watetezi Kabras Sugar walinyoa majirani zao na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Masinde Muliro (Mmust) 21-0 baada ya kuongoza kwa alama hizo wakati wa mapumziko mjini Kakamega.

Menengai Oilers walikomoa Homeboyz 37-24 uwanjani Jamhuri Park baada ya kuongoza 14-8. Ligi sasa imeenda mapumzikoni kwa sababu ya likizo ya Krismasi hadi Januari 7, 2023.

  • Tags

You can share this post!

KOMBE LA DUNIA FIFA 2022: Mbivu na mbichi kuhusu nani mkali...

DARUBINI YA WIKI: Toleo Nambari 16 | Desemba 18, 2022

T L