• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 AM
Real Madrid wazamisha Getafe na kupaa hadi kileleni mwa jedwali la La Liga

Real Madrid wazamisha Getafe na kupaa hadi kileleni mwa jedwali la La Liga

Na MASHIRIKA

REAL Madrid walirejea kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) baada ya kutandika Gatafe 1-0 mnamo Jumamosi usiku ugani Coliseum Alfonso Perez.

Eder Militao alifunga bao la pekee katika mchuano huo baada ya kukamilisha mpira wa kona kutoka kwa kiungo mzoefu Luka Modric katika dakika ya tatu.

Bao la pili la Real lilifutiliwa mbali baada ya teknolojia ya VAR kubaini kuwa Rodrygo alikuwa ameotea alipomzidi ujanja kipa wa Getafe, David Soria.

Real walipokonywa pia mkwaju wa penalti baada ya kubainika kuwa mpira ulikuwa umetoka nje ya uwanja kabla ya Vinicius Junior kukabiliwa na Luis Milla visivyo ndani ya kijisanduku.

Getafe walipoteza nafasi kadhaa za kusawazisha mambo kupitia kwa Borja Mayoral na Fabrizio Angileri katika kipindi cha pili.

Real kwa sasa wanajivunia alama 22, tatu kuliko nambari mbili Barcelona ambao watavaana na Celta Vigo mnamo Oktoba 9, 2022. Gatafe wanakamata nafasi ya 16 kwa pointi saba sawa na Girona, Almeria na Valladolid.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

PENZI LA KIJANJA: Usiwekeze hisia bila uhakika wa nia ya...

BAHARI YA MAPENZI: Uhusiano ukidorora, hisia nazo huyoyoma

T L