• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Red Star Belgrade yaweka benchi Mkenya Odada ikizidi kutetemesha Ligi Kuu

Red Star Belgrade yaweka benchi Mkenya Odada ikizidi kutetemesha Ligi Kuu

Na GEOFFREY ANENE

Red Star Belgrade anayochezea kiungo Mkenya Richard Odada ilidumisha rekodi ya kutoshindwa hadi mechi 26 katika mashindano yote baada ya kulipua TSC Backa Topola 3-1 kwenye Ligi Kuu ya Serbia, Jumatano.

Odada,20, ambaye alionja dakika zake za kwanza kwenye ligi hiyo ya klabu 20 dhidi ya Proleter mnamo Februari 28 alipochezeshwa dakika 31, hakutumiwa Jumatano. Alikuwa kwenye benchi.

Red Star ya kocha Dejan Stankovic ilizoa ushindi huo wake wa 12 mfululizo ligini baada ya kupata mabao kutoka kwa Milan Pavkov dakika ya 54 na 71 na Guelor Kanga aliyejaza kimiani penalti dakika ya 68.

Mabingwa hao wa Serbia walisalia watu 10 dakika ya 57 baada ya Milan Gajic kusababisha penalti na kuonyeshwa kadi nyekundu. Mshambuliaji wa Backa Topola, Nenad Lukic alifuma wavuni penalti hiyo akifanya mabao kuwa 1-1 kabla ya Kanga kurejesha Red Star kifua mbele 2-1 alipopachika penalti iliyopatikana Sasa Tomanovic alipolishwa kadi yake ya pili ya njano.

Red Star inaongoza kwa alama 68 kutokana na ushindi 22 na sare mbili. Inafuatwa alama sita nyuma na mahasimu wao wakuu Partizan Belgrade ambao wamesakata michuano 25. Mechi ya Red Star ijayo ni Machi 7 dhidi ya nambari tatu Cukaricki iliyovuna alama 51 baada ya kujibwaga uwanjani mara 25.

  • Tags

You can share this post!

Chanjo ya corona hatarini

Kampeni chanjo ya corona ipewe wanamichezo wa Kenya...