• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Sande Katumba analenga kuchezea AFC Leopards

Sande Katumba analenga kuchezea AFC Leopards

Na JOHN KIMWERE

STRAIKA wa Equity Bank FC raia wa Uganda, Sande Katumba amesema kuwa anatamani sana kusakatia klabu kongwe nchini ya AFC Leopards ambayo hushiriki ngarambe ya Ligi Kuu ya Betking Kenya Premier League (BKPL).

Mshambuliaji huyo aliibuka mchezaji muhimu kwa Equity Bank ambayo hushiriki mechi za Kundi A Ligi ya Taifa Daraja la Kwanza kwenye mechi za kuwania taji la Betway Cup.

Katumba ndiye aliyetupia kambani goli la pekee lilisaidia Equity Bank kushinda mabingwa watetezi, Bandari FC kwa bao 1-0 katika robo fainali.

Hata hivyo, Equity Bank ilibanduliwa na Ingwe kutoka kipute hicho kwenye mechi ya nusu fainali ilipozabwa mabao 6-5 kupitia mipigo ya penalti baada ya kutoka sare tasa.

”Kusema ukweli nimekuwa nikitamani tena sana kuvalia jezi ya Ingwe ambapo hatua ya kucheza na wachezaji hao imenitia ari ya kulenga kuchezea klabu za haiba kubwa nchini,” akasema na kuongeza kuwa atazidi kujituma kwa udi na uvumba akilenga kutimiza azma yake kuchezea klabu hiyo miaka ijayo.

Katumba anajivunia kuchezea Nairobi City Stars maarufu kama Simba wa Nairobi ilipokuwa ikishiriki Ligi Kuu ya Kenya kabla ya kushushwa ngazi na kupanda tena.

You can share this post!

Kituo cha afya cha Kiandutu sasa kutoa huduma bora za...

Momanyi na Syombua waongoza Moraa na Kipruto kuweka rekodi...