• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
Timu 5 zawinda huduma zake Kahiro wa FC Talanta

Timu 5 zawinda huduma zake Kahiro wa FC Talanta

NA JOHN KIMWERE

KLABU tano za Ligi Kuu Nchini (FKF-PL) zinawinda huduma za mchana nyavu shupavu, Francis Kahiro ambaye husakatia FC Talanta ya kocha Ken Kenyatta.

Timu hizo zilivutiwa na mchezaji huyo mwezi Okotoba 2021 alipotingia FC Talanta mabao mawili na kuisaidia kuzoa ushindi wa 2-0 dhidi ya Tusker FC.

Baadaye alifanikiwa kutikisa nyavu mara saba na kuibuka mfungaji bora wa kikosi hicho kwa mabao tisa.

Duru zaeleza kuwa klabu zinazofukuzia huduma zake ni mabingwa wa ligi kuu mara nne, Maafande wa Ulinzi Stars, Sofapaka FC, Kariobangi Sharks, KCB na Posta Rangers.

”Fowadi huyo alionyesha mchezo mzuri kwenye kampeni za msimu uliyopita ambapo klabu hizo tayari zimeonyesha nia ya kutwaa sajili yake,” duru zimesema.

Mchezaji huyo ana mkataba wa kuchezea klabu hiyo hadi mwezi Septemba 2023.

Kwingineko, kiungo wa Harambee Stars Eric Johanna Omondi amevunja ndoa yake na klabu ya Beveren FC ya Ubelgiji.

Licha ya kusajiliwa na klabu hiyo kwa kipindi cha miezi sita alishindwa kuonyesha mchezo wa kuvutia ambapo alifanikiwa kuichezea kwa muda wa dakika saba pekee.

Mwanasoka huyo aliyewahi kupigia Mathare United alijiunga na klabu hiyo akitokea Jonkopings Sodra ya Uswidi.

  • Tags

You can share this post!

Waliokuwa maafisa wa serikali ya Kidero wahukumiwa miaka 30...

Silva asihi Neymar ahamie Chelsea

T L