• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 6:50 AM
Uingereza na Wales katika makundi ya kifo droo ya Uefa Nations League ikifanyika

Uingereza na Wales katika makundi ya kifo droo ya Uefa Nations League ikifanyika

Na MASHIRIKA

UINGEREZA watavaana na Italia waliowapiga katika fainali ya Euro 2020 kisha Ujerumani katika hatua ya makundi ya Uefa Nations League 2022-23.

Wales kwa upande wao wametiwa katika zizi moja na Poland, Ubelgiji pamoja na Uholanzi.

Chini ya kocha Gareth Southgate, Uingereza wako katika Kundi A3 ambalo pia linajumuisha Hungary.

Scotland watapambana na Jamhuri Ireland, Armenia na Ukraine katika Kundi B1.

Northern Ireland wametiwa katika Kundi C2 kwa ajili ya mapambano hayo ambayo yameratibiwa kuanza Juni 2, 2022. Kikosi hicho cha mkufunzi Ian Baraclough kitamenyana na Ugiriki, Kosovo na ama Cyprus au Estonia ambao lazima wavaane mwanzo kwenye mchujo wa Machi 2022 kabla ya kuingia hatua ya makundi.

Mabingwa watetezi Ufaransa wako katika Kundi A1 kwa pamoja na Denmark, Austria na Croatia. Ureno na Uhispania ambao ni majirani wamepangwa pamoja na Jamhuri ya Czech na Uswisi katika Kundi A2.

Kila kikosi lazima kicheze mechi nne za makundi kati ya Juni 2 na Juni 14 kabla ya kutandaza mechi mbili za mwisho kuanzia Septemba 22-27, 2022.

Washindi wanne wa kwanza kutoka kila mojawapo ya makundi ya League A watachuana kwenye fainali za Juni 2023. Uingereza walizidiwa maarifa na Italia kupitia penalti kwenye fainali ya Euro 2020 uwanjani Wembley, London mnamo Julai 2021.

MAKUNDI YA UEFA NATIONS LEAGUE:

KUNDI A1: Austria, Croatia, Denmark, France.

KUNDI A2: Czech Republic, Switzerland, Portugal, Spain.

KUNDI A3: Hungary, England, Germany, Italy.

KUNDI A4: Wales, Poland, Netherlands, Belgium.

KUNDI B1: Ukraine, Scotland, Republic of Ireland, Armenia

KUNDI B2: Iceland, Russia, Israel, Albania

KUNDI B3: Bosnia-Herzegovina, Finland, Romania, Montenegro

KUNDI B4: Sweden, Norway, Serbia, Slovenia

KUNDI C1: Turkey, Luxembourg, Lithuania, Faroe Islands

KUNDI C2: Northern Ireland, Greece, Kosovo, Cyprus/Estonia*

KUNDI C3: Slovakia, Belarus, Azerbaijan, Kazakhstan/Moldova*

KUNDI C4: Bulgaria, North Macedonia, Georgia, Gibraltar

KUNDI D1: Liechtenstein, Kazakhstan/Moldova*, Andorra, Latvia

KUNDI D2: Malta, Cyprus/Estonia*, San Marino

*Kazakhstan watacheza dhidi ya Moldova nao Cyprus wamenyane na Estonia katika mchujo wa Machi 2022. Washindi watakwezwa hadi League C huku watakaopoteza wakisalia League D

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

TUSIJE TUKASAHAU

Niliitwa kusaidia utekelezaji wa mauaji ya wakili...

T L