• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 12:48 PM
Vipusa wa Man-City wadengua mabingwa watetezi Manchester City kwenye nusu-fainali ya League Cup

Vipusa wa Man-City wadengua mabingwa watetezi Manchester City kwenye nusu-fainali ya League Cup

Na MASHIRIKA

STINA Blackstenius alifunga bao la pekee na la ushindi katika muda wa ziada na kusaidia Arsenal kupepeta mabingwa watetezi Manchester City 1-0 na kufuzu kwa fainali ya Continental League Cup.

Blackstenius alijaza kimiani krosi ya Lina Hurtig katika dakika ya 93 na kuweka waajiri wake pua na mdomo na taji la kwanza tangu watazwe malkia wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) mnamo 2018-19.

Kichapo hicho kilifuta rekodi ya kutopigwa kwa Man-City katika mechi 16 mfululizo. Ilikuwa mara ya kwanza kwa kikosi hicho kuangushwa tangu Septemba 2022.

Arsenal ambao ni mabingwa mara tano wa League Cup, sasa watavaana na West Ham United au Chelsea kwenye fainali itakayochezewa ugani Selhurst Park mnamo Machi 5, 2023. Wawili hao watamenyana katika nusu-fainali ya pili mnamo Alhamisi ya Februari 9, 2023.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Vitushi katika hadithi fupi ‘Mapambazuko’

NGUVU ZA HOJA: Vyuo anuwai vitumie sasa Kiswahili kufunzia...

T L