• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
Vipusa wa Ufaransa sasa kuvaana na Uholanzi kwenye robo-fainali za Euro baada ya kukomoa Ubelgiji katika Kundi D

Vipusa wa Ufaransa sasa kuvaana na Uholanzi kwenye robo-fainali za Euro baada ya kukomoa Ubelgiji katika Kundi D

Na MASHIRIKA

UFARANSA walitinga robo-fainali za Euro za Wanawake wakisalia na mechi moja zaidi katika Kundi D baada ya kupepeta Ubelgiji 2-1 mnamo Alhamisi usiku ugani New York, Uingereza.

Chini ya kocha Corinne Diacre, Ufaransa walishuka dimbani kwa ajili ya mechi hiyo wakijivunia ushindi mnono wa 5-1 dhidi ya Italia katika gozi la ufunguzi.

Kadidiatou Diani alishirikiana vilivyo na Sakina Karchaoui katika dakika ya sita na kuwaweka Ufaransa kifua mbele.

Bao hilo la mapema lilirejesha kumbukumbu za mechi iliyotangulia dhidi ya Italia ambapo mabao yote yaliyofungwa na Ufaransa yalifumwa wavuni katika kipindi cha kwanza.

Ubelgiji waliomtegemea zaidi kipa Nicky Evrard, walisawazishiwa na Janice Cayman katika dakika ya 36, muda mfupi kabla ya Griedge Mbock Bathy kufungia Ufaransa bao la ushindi.

Ubelgiji walikamilisha mechi na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya Amber Tysiak kuonyeshwa kadi nyekundu kwa utovu wa nidhamu na kunawa mpira ndani kijisanduku. Penalti iliyotokana na tukio hilo ilipotezwa na Wendy Renard wa Ufaransa.

Ufaransa sasa wanaselelea kileleni mwa Kundi D kwa alama sita, nne zaidi kuliko Iceland huku Italia na Ubelgiji wakiwa na alama moja kila mmoja. Ufaransa watavaana na Uholanzi kwenye robo-fainali baada ya kikosi hicho kuambulia nafasi ya pili kwenye mapambano ya Kundi C.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

CECIL ODONGO: Ruto auze sera na kufafanua yaliyomo kwenye...

Pigo baada ya Chebukati kukataa orodha ya wabunge, maseneta...

T L