• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:07 PM
Wachezaji wawili wa Harambee Starlets wajiunga na Sethu FC nchini India

Wachezaji wawili wa Harambee Starlets wajiunga na Sethu FC nchini India

NA AREGE RUTH

NAHODHA wa Harambee Starlets Dorcus Shikobe Nixon na kiungo mshambuliaji wa Starlets Omondi Ivy Faith, wamejiunga na klabu inayoshiriki Ligi  ya Daraja la Juu nchini India, Sethu FC.

Kabla ya kuhamia India, Shikobe, 33, alikuwa akicheza soka ya kulipwa huko Cyprus akiwajibikia Lakatamia FC. Alijiunga na timu hiyo mwaka 2021. Pia, aliwahi kuchezea timu ya Oserian Ladies ambayo iliwahi kucheza Ligi Kuu ya Wanawake Nchini (KWPL). Amejiunga na Sethu FC kwa muda usiojulikana. Ndiye nahodha wa Starlets. Yeye ni mmoja wa wachezaji wa kutegemewa na bora ambao Kenya imewahi kutoa. Beki huyo, alikuwa kwenye kikosi ambacho kiliwakilisha Kenya katika Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (AWCON) mwaka 2016.

Kwa upande mwingine, Faith anajiunga na timu hiyo akitokea Wadadia Women ya KWPL. Mnamo Desemba 03, 2022, kupitia kurasa zake za kijamii, aliaga timu yake rasmi.

“Naandika kuishukuru timu hii ambayo itabaki kuwa moyoni mwangu siku zote. Tangu nilipojiunga na timu hii imekuwa ya msaada mkubwa kwangu. Asante benchi ya ufundi, uongozi na wachezaji wote kwa ujumla,” aliandika Faith kwenye kurasa za kijamii.

Mwezi Aprili 2022, alituzwa kuwa mchezaji bora wa mwezi na Chama cha Ustawi wa Wanasoka wa Kenya (KEFWA). Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 alipata kura 31 kushinda tuzo hiyo, akifuatiwa na Cindy Ngaira wa Ulinzi Starlets na Belinda Christine kutoka Kisumu All Starlets waliopata kura 25 na 22 mtawalia. Alienda nyumbani na kombe la kibinafsi na tuzo ya pesa yenye thamani ya Sh10,000.

Sethu FC ni klabu ya soka ya wanawake ya Kihindi yenye makao yake Madurai, Tamil Nadu, ambayo inashiriki Ligi ya Wanawake ya India. Walinyanyua kombe la ligi mnamo 2018-19.

Ligi hiyo pia ni nyumbani kwa Mkenya mshambuliaji Elizabeth Katungwa anayechezea timu ya Royal Rangers.

  • Tags

You can share this post!

Wakazi wa Nairobi wafurika Lunar Park kujivinjari wakati wa...

Claudio Ranieri arejea Italia kuwa kocha wa klabu ya...

T L