• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 6:40 PM
Karugu ataka madiwani wazuiwe kumtimua ofisini

Karugu ataka madiwani wazuiwe kumtimua ofisini

Na MERCY MWENDE

NAIBU gavana wa Kaunti ya Nyeri, Caroline Karugu anataka bunge la kaunti hiyo kuzuiliwa kujadili ombi la kumuondoa ofisini.

Katika kesi aliyowasilishwa katika Mahakama ya kutatua mizozo baina ya wafanyikazi na waajiri, Bi Karugu alisema kesi hiyo tayari iko mbele ya korti na haifai kuzungumziwa katika majukwaa mengine.

Kulingana naye, baadhi ya maswala yanatarajiwa kujadiliwa yamo katika kesi iliyosajiliwa kortini kama ELRC wa 2021.

Katika kesi hiyo ambayo katibu wa kaunti hiyo, Benjamin Gachichio na Gavana Mutahi Kahiga ni washtakiwa, Bi Karugu anawalaumu kwa kukosa kumlipa mshahara wake na marupurupu tangu 2019.

You can share this post!

Kiraitu atwaa uongozi chama kipya Mlimani

Ruto, Muturi wasuta mabwanyenye wa MKF kwa kudai ndio wenye...