NA SIAGO CECE
KATIBU wa idara ya serikali ya urekebishaji tabia, Bi Safina Kwekwe, ameahidi kuendelea kumpigia debe Prof Hamadi Boga kwa ugavana Kwale.
Bi Kwekwe alitarajiwa kuwa mgombea mwenza wa Prof Boga lakini barua yake ya kujiuzulu serikalini ilikataliwa.
“Niliombwa na wakuu wangu kubaki ofisini kwa sababu kuna majukumu niliyotakikana kukamilisha,” akaeleza.
Prof Boga alimteua Bw Nurrein Mwatsahu kuwa mgombea mwenza wake.