Na SHABAN MAKOKHA
WANDANI wa Kinara wa ODM Raila Odinga wameanza kampeni kali ya kumuuza Magharibi mwa nchi na wikendi iliyopita walitua katika Kaunti ya Busia ambapo walimtaja kama anayefaa zaidi kuingia ikulu 2022.
Naibu Kiongozi wa ODM, ambaye pia ni Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya pamoja na Wabunge Raphael Wanjala (Budalang’i), Kizito Mugali (Shinayalu), Godfrey Osotsi (maalum) na mbunge wa zamani wa Funyula Paul Otuoma, walimtaja Bw Odinga kama mwanamageuzi ambaye anastahili kuchukua uongozi wa nchi baada ya Rais Uhuru Kenyatta kustaafu mwakani.
Kinara wa ANC Musalia Mudavadi na mwenzake wa Ford Kenya Moses Wetang’ula ambao wanatoka Magharibi mwa nchi pia wametangaza kuwa watawania kiti cha Urais 2022.