NA LUCY MKANYIKA
MBUNGE wa Mwatate, Bw Andrew Mwadime, amekashifu Chama cha Communist (CPK) kwa kujiunga na Naibu Rais William Ruto.
Mbunge huyo aliondoka CPK dakika za mwisho na kuwa mgombeaji huru wa ugavana Taita Taveta.
Alisema walikuwa wamekubaliana chama hicho kisingeingia katika muungano wowote.
Hata hivyo, hakufafanua kama atamuunga mkono kinara wa ODM, Bw Raila Odinga kuwania urais.