NA ANTHONY KITIMO
BAADA ya kung’olewa katika kiti cha ubunge Ganze 2017, Bw Peter Safari Shehe, aliamua kuwania udiwani mwaka huu, na kufaulu kushinda.
Bw Shehe, ambaye alitangazwa mshindi wa udiwani Wadi ya Jaribuni, alikuwa mbunge mwaka wa 2013 hadi 2017.
Alisema aliamua kuwania udiwani mwaka huu ili kujiandaa kuwania kiti kingine kikubwa katika miaka ijayo.
Kulingana naye, uamuzi wa kuwania udiwani ulitokana na mashauriano aliyofanya na wakazi.