Na RUTH MBULA
CHAMA kipya cha United Progressive Alliance (UPA), kimeanza kujivumisha na kudhamini wawaniaji wa viti tofauti katika kaunti za Kisii, Nyamira na maeneo mengine nchini.
Gavana wa Nyamira, Bw Amos Nyaribo tayari amejiunga na chama hicho na kutangaza kwamba atakitumia kutetea kiti chake.
Chama hicho kinashirikiana Muungano wa Azimio la Umoja linaloongozwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga.