Na GEORGE ODIWUOR
ALIYEKUWA Gavana wa Nairobi Evans Kidero (pichani), amewahimiza wakazi wa Homa Bay kujiandikisha kwa wingi kuwa wanachama wa ODM ili wakubaliwe kushiriki katika kura za mchujo za chama hicho Aprili.
Dkt Kidero ambaye alikuwa akiendesha kampeni za kutoa uhamasisho kuhusu uchaguzi, alisema katika miaka ya nyuma wananchi wamekuwa wakikangayikiwa wasijue la kufanya wakati wa kupiga kura.