NA WINNIE ATIENO
MBUNGE wa Kisauni, Bw Ali Mbogo (pichani), amedai kuwa aliyekuwa gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko, anaandamwa kwa vile wapinzani wake wameanza kubabaika akiwania ugavana Mombasa.
“Wanajua Mbogo na Sonko wameshashinda ndio maana wakakimbia kortini lakini haki haizami. Lengo letu ni kusaidia maskini. Watu wa Mombasa wameamua na hakuna kurudi nyuma,” akasema Bw Mbogo.