• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Vijana waapa kuunga Raila

Vijana waapa kuunga Raila

Na KENYA NEWS AGENCY

ZAIDI ya vijana 2,000 kutoka maeneobunge yote ya Kaunti ya Nyamira wamejitokeza na kusema kuwa wataunga mkono azma ya kuwania urais ya kinara wa ODM Raila Odinga.

Vijana hao walikongamana mjini Kebirigo mnamo Jumatatu.

walisema kuwa Bw Odinga ndiye kiongozi mwenye maono bora zaidi nchini na watahakikisha kuwa anapata uungwaji mkono kutoka kwa wakazi wengi wa kaunti hiyo.

Kiongozi wa Kitaifa wa Vijana wa ODM John Ketora alitoa wito kwa vijana wengi hasa katika ngome za Bw Odinga wajitokeze na kujisajili kama wapigakura kwa kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kuchangia katika kuwachagua viongozi bora.

“Raila ana historia ya kupigania maslahi ya raia kwa hivyo tuna hakika kuwa akipata uongozi masuala ambayo amekuwa akiapigania yatatekelezwa,” akasema Bw Ketora.

You can share this post!

Jowie alijipiga risasi akadai kushambuliwa – korti...

Museveni akemea mapinduzi Burkina Faso

T L