• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 8:50 AM
Vijana wazima Sonko mkutano wa Azimio

Vijana wazima Sonko mkutano wa Azimio

NA ANTHONY KITIMO

POLISI walilazimika kufyatua risasi hewani kumuokoa aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko kutoka kwa vijana waliomzuia kuhudhuria mkutano wa kampeni wa Azimio la Umoja One Kenya ambao ulihutubiwa na mgombea urais wa muungano huo Raila Odinga mjini Mombasa.

Vijana hao walizuia gari la Bw Sonko aina ya Toyota Alto kuingia katika uwanja wa Mkomani, Mombasa.

Viongozi wawili kati ya watatu ambao majina yao yaliwasilishwa kwa Bw Odinga na kamati iliyohoji wanaomezea mate wadhifa wa naibu wake iwapo atashinda uchaguzi mkuu ujao walihudhuria mkutano huo huku waziri mkuu huyo waza zamani akitarajiwa kutaja mwaniaji mwenza wake leo Jumapili.

Wawili hao ni kiongozi wa chama cha Narc Kenya Martha Karua na aliyekuwa mbunge wa Gatanga Peter Kenneth.

Mwakilishi wa wanawake kaunti ya Murang’a Sabina Chege pia alihudhuria.Kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka hakuwepo.

Sonko anagombea ugavana kaunti ya Mombasa kwa tikiti ya chama cha Wiper.

Tukio la Jumamosi lilijiri saa chache baada ya Bw Odinga kupatanisha viongozi wote ili waruhusu wawakilishi wote wa Azimio kuhudhuria mkutano huo.

  • Tags

You can share this post!

Nitakuwa na mshauri maalum wa masuala ya wanawake, Nassir...

Kalonzo akaa ngumu, atishia kuwania urais

T L