• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
Pendekezo la kubadilisha Katiba lagawanya Jubilee

Pendekezo la kubadilisha Katiba lagawanya Jubilee

Na WANDISHI WETU

PENDEKEZO la kinara wa ODM Raila Odinga kutaka Katiba ifanyiwe mabadiliko limegawanya chama cha Jubilee.

Kile kimejitokeza ni kuwa wabunge wa uliokuwa mrengo wa TNA wanataka mabadiliko huku wa URP wakipinga.

Miongoni mwa waliojitokeza kuunga mkono ni Mbunge Maalum Maina Kamanda, Moses Kuria (Gatundu Kusini), Michael Muchira (Ol-Joro Orok, Kinuthia Gachobe (Subukia), Kimani Kuria (Molo), Bi Faith Gitau (Mwakilishi wa Kike wa Nyandarua), Patrick Mariru (Laikipia Magharibi), Patrick Munene (Chuka-Igamba-Ng’ombe) na Bw Peter Kimari (Mathioya).

Wabunge hao wanasema kubadilisha Katiba kutasaidia kupunguza mzigo wa kulipa ushuru wa juu.

Lakini Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen amepuuzilia mbali wito wa kuandaa kura ya maamuzi.

Bw Murkomen ambaye ni Kiongozi wa Wengi katika Seneti alisema wanaopigania kufanyika kwa kura ya maamuzi wanaongozwa na masilahi ya kibinafsi.

“Wanaotaka Katiba ifanyiwe mabadiliko wanataka kufanya hivyo ili waweze kujipatia nafasi ya kuingia mamlakani 2022,” akasema.

Wakati huo huo, kiongozi wa Ford Kenya Moses Wetang’ula ameunga mkono pendekezo hilo la Bw Odinga huku akisema kuwa Katiba inafaa kufanyiwa marekebisho ili fedha zinazotolewa kwa serikali za kaunti ziongezwe kutoka asilimia 15 hadi asilimia 45 ya bajeti ya kitaifa.

Ripoti ya Patrick Lang’at, Florah Koech na Steve Njuguna

You can share this post!

Jeshi lamulikwa kwa ununuzi wa ndege kuukuu

Taharuki Raila akipiga kambi mjini Migori

adminleo