• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 11:13 AM
HONGO: Muturi atembelea vyoo vya wanawake bungeni kujua ukweli

HONGO: Muturi atembelea vyoo vya wanawake bungeni kujua ukweli

NA CHARLES WASONGA

SPIKA wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi Jumanne aliongoza wanachama wa kamati ya bunge inayochunguza madai ya wabunge kuhongwa kuangusha ripoti kuhusu sakata ya sukari, katika ziara ya vyoo vya wanawake bungeni kuthibitisha habari kuwamba baadi ya wabunge waliweza kujadili suala hilo humo.

Bw Muturi aliandamana na zaidi ya wabunge 10 ambao ni wanachama wa Kamati ya Bunge kuhusu Hadhi ya Mamlaka pamoja na  Mbunge Mwakilishi wa Wanawake wa Kiambu Gathoni Wa Muchomba ambaye kukagua vyoo hivyo.

Majuma mawili yaliyopita Bi Wa Muchomba  aliambia kamati hiyo kwamba aliwasikiza wabunge wenzake wa kike wakijadiliana chooni jinsi walivyohongwa na Mbunge Mwakilishi wa Wajir Fatuma Gedi ili waaungushe ripoti hiyo, ambayo ilielekeza kidole cha lawama kwa mawaziri Henry Rotich (Fedha) na Adan Mohammed (Masuala ya Afrika Mashariki).

Bi Wa Muchomba alidai alikuwa ndani ya choo cha wanawake kilichoko karibu na lango la kuingia ndani ya ukumbi wa bunge alipowasikia wenzake wawili, ambao hawawatambua kwa majina wala kuwaona, wakijadiliana ndani ya choo jinsi walivyohongwa kwa kati ya Sh10,000 na Sh30,000 ili kuzima ripoti hiyo.

Ripoti hiyo iliandaliwa na kamati ya pamoja ya bunge kuhusu Biashara na Kilimo iliyoongozwa na Mbunge wa Kieni Kanini Kega na mwenzake wa Mandera Kusni Adan Haji.

Hapo ndipo kamati hiyo iliamua kwamba Mbunge huyo wa Kiambu angeandamana nao ili aonyeshe wanachama wake mahala ambapo alikuwa amesimama akisikiza wenzake wakijadiliana kuhusu kupokea mlungula.

Hata hivyo walinzi wa bunge waliwazuia wanahabari kuandamana na wanachama wa kamati hiyo katika uchunguzi huo.

Ripoti hiyo ilipendekeza kuwa Mbw Roticha na Adan pamoja na aliyekuwa Waziri wa Kilimo Willy Bett wachunguzwa na Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) kwa kuruhusu uingizwaji wa sukari ya magendo humu nchini.

Bunge lilikataa kupitisha ripoti hiyo kwa madai kuwa ilifeli kuelezea waziwazi kama kulikuwa na sukari yenye sumu katika masoko ya humu nchini. Vile vile, wabunge walidai kuwa kamati hiyo ilifeli kuwajibisha asasi husika kama vile Shirika la Kukagua Ubora wa Bidhaa (KEBs) kwa kuhusu sukari isiyo salama kwa afya kuingizwa humu nchini.

Kufikia sasa kamati hiyo ambayo mwenyekiti wake ni Bw Muturi imewahoji jumla ya wabunge kumi (10) kuhusiana na madai kuwa wenzao walihonjwa ili kukataa ripoti hiyo.

Wabunge ambao walihojiwa na kamati hiyo ni pamoja na; Didmus Barasa (Kimilili), James Onyango K’Oyoo (Muhoroni), Samuel Atandi (Alego Usonga), Simba Arati (Dagoreti Kaskazini), John Waluke  (Sirisia) na Geoffrey Odanga (Matayos).

Wengine ni; Rahab Mukami (Mbunge Mwakilishi wa Nyeri), Ayub Savula (Lugari), Justus Murunga (Matungu), Godffrey Osotsi (Mbunge Maalum), Jane Kihara (Naivasha), David Gikaria (Nakuru Mjini Mashariki) na Joseph Tonui (Kuresoi Kusini).

Wengi wao walikana kuwahi kuona wenzao wakihongwa au wao wenyewe kupokezwa pesa za hongo ili kuwashawishi waangushe ripoti hiyo.

You can share this post!

REFERENDA: Wabunge kuamua kuhusu terehe ya uchaguzi

Jacque Maribe na Jowie warudishwa rumande hadi Oktoba 24

adminleo