• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
Wabunge wa kike wa Jubilee wamtaka Rais kuitisha mkutano wa Kundi la Wabunge

Wabunge wa kike wa Jubilee wamtaka Rais kuitisha mkutano wa Kundi la Wabunge

Na CHARLES WASONGA

WABUNGE wa kike wa chama cha Jubilee wamemtaka Rais Uhuru Kenyatta kuitisha mkutano wa Kundi la Wabunge (PG) kujadili migawanyiko ndani ya Jubilee.

Wabunge hao ni wawakilishi wa Wanawake wa kaunti kadha na wengine wa maeneobunge.

Rahab Mukami (Nyeri), Sabina Chege (Murang’a), Faith Gitau (Nyandarua), Joyce Korir (Bomet) na mbunge wa Maragua Mary Njoroge, walisema Jumanne wangetaka Rais Uhuru Kenyatta awaelezee katika mkutano huo ikiwa kuna mabadiliko katika mkataba kati yake na Naibu wake William Ruto.

Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Murang’a katika Bunge la Kitaifa Bi Sabina Chege. Picha/ Maktaba

Walielezea hofu kwamba ufa ndani ya Jubilee unaendelea kupanuka kila uchao wafuasi wa Dkt Ruto wakiendelea kushambuliana na wapinzani wao, wanaojiita Kieleweke.

“Chama cha Jubilee ni kinaunga na tunasimama nyuma ya Rais na naibu wake na tutaendelea kuwaunga mkono bila kuwaogopa wanaoututisha,” Bi Chege akasema mjini Nyeri wakati wa mkutano wa kundi la wanawake wa Kanisa la PCEA, Nyamakia kaunti ya Nyeri.

Lawama

Wakiongea katika mkutano wa kundi la wanawake la Nyamachaki PCEA Women Guild wabunge hao waliwalaumu wenzao Kieleweke kwa migawanyiko inayoshuhudiwa katika chama hicho.

“Ikiwa mgawanyiko katika Jubilee ni rasmi basi kiongozi wetu Rais Kenyatta anafaa kuwajulisha wanachama kupitia mkutano wa PG.

Bila kuwataja majina, wabunge hao walidai kuwa baadhi ya wenzao kutoka Mlima Kenya ndio wanachochea uhasama ndani ya Jubilee kwa kudai kuwa wandani wa Ruto wanamsaliti Rais Kenyatta.

“Tunataraji kwamba Rais ataongozwa na busara na kukoma kukoma kuwasikiliza wale ambao wanaongozwa na chuki,” akasema Bi Chege.

Bi Njoroge alisema eneo la Mlima Kenya lilimpia kuta Rais Kenyatta na Ruto kwa wingi akiongeza kuwa kiongozi wa taifa aliwapa wabunge ruhusa ya kufanyakazi kwa ukaribu na naibu rais.

“Sasa wanatuambia kwamba tukionekana na Naibu Rais hiyo inaonyesha kuwa tunampinga Rais. Nini kimebadilika. Rais anafaa kuitisha mkutano wa PG ili atoe tangazo rasmi kwamba kuna mgawanyiko,” akaeleza.

“Eneo la Mlima Kenya halitamsaliti Naibu Rais,” Bi Njoroge akaongeza.

Bi Korir na Bi Gitau walishikilia kuwa hawata hawatakoma kumuunga azma ya Dkt Ruto ya kuwania urais eti kwa sababu wamepokonywa walinzi.

You can share this post!

BONGO LA BIASHARA: Sh100 za chama kila wiki zajengea...

Wanaobadilisha mikondo ya mito eneo la Mlima Kenya waonywa...

adminleo