• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 11:13 AM
Magufuli apiga marufuku maandamano nchini mwake

Magufuli apiga marufuku maandamano nchini mwake

DAR ES SALAAM, Tanzania

RAIS wa Tanzania John Pombe Magufuli amepiga marufuku maandamano yoyote yasiyoidhinishwa na serikali yake.

Akiongea katika mkutano wa hadhara kaskazini mwa Tanzania, kiongozi huyo Ijumaa alionya kuwa yeyote atakayedhubutu kupanga na kushiriki maandamano, haswa ya kupinga utawala wake, ataadhibiwa vikali.

Alisema maandamano kama hayo ya kisiasa huathiri mkondo wa mageuzi ya kiuchumi aliyoanzisha pamoja na vita dhidi ya ufisadi.

Tangu Bw Magufuli alipoinga mamlakani mnamo Novemba 2015, serikali yake imeanzisha mageuzi ya kiuchumi na vita vikali dhidi ya ufisadi.

You can share this post!

JAMVI: Raila apania kujaribu bahati yake Ikulu kwa mara ya...

Kirwa, Cheshari na Kosgei kushiriki Hannover Marathon

adminleo