Na MASHIRIKA
NORWICH City waliteremshwa ngazi kwenye Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu baada ya kupokezwa kichapo cha 2-0 kutoka kwa Aston Villa mnamo Jumamosi uwanjani Villa Park.
Kushushwa huko kwa Norwich kuthibitishwa na ushindi wa 2-1 uliosajiliwa na Burnley dhidi ya Watford ugani Vicarage Road. Norwich kwa sasa wanavuta mkia wa jedwali la EPL kwa alama 21 baada ya mechi 34 ambazo pia zimetandazwa na Burnley wanaokamata nafasi ya 19 kwa pointi 22.
Ollie Watkins aliwaweka Villa kifua mbele katika dakika ya 41 kabla Danny Ings kupachika wavuni bao la pili mwishoni mwa kipindi cha pili. Villa waliokomoesha rekodi duni ya kutoshinda mechi yoyote kati ya tano za awali, sasa wanashikilia nafasi ya 13 kwa alama 40 sawa na Brentford na Southampton.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO