• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
Ndege nne za Jambojet kuimarisha safari Afrika

Ndege nne za Jambojet kuimarisha safari Afrika

Na BERNARDINE MUTANU

KAMPUNI ya Jambojet imepanga kununua ndege nne katika muda wa miezi 18 ijayo kwa lengo la kuimarisha operesheni zake nchini na katika eneo la Afrika.

Mkurugenzi Mku wa Jambojet Willem Hondiusa alitangaza mpango huo Alhamisi, Entebbe, Uganda, wakati wa kuzindua safari ya kwanza ya ndege ya kampuni hiyo kimataifa.

Jambojet ni tawi la Kenya Airways na inatarajia kununua ndege mbili zilizotumiwa aina ya Bombadier Q400 kufikia Juni 2018 na zingine mbili mpya mapema 2019.

Bw Hondius alisema serikali kwa niaba ya Jambojet imetuma ombi kwa ndege hiyo kuidhinishwa kuanza ziara zake Rwanda, Ethiopia, Sudan, Congo, Tanzania na Burundi.

“Maombi yalitumwa Oktoba 2017 na tunatumainia kuwa kufikia mwisho wa mwaka, tutakuwa tumeanza safari zetu katika mataifa mawili,” alisema wakati wa mahojiano na wanahabari Entebbe, Uganda.

Kampuni hiyo ikinunua ndege nne, itakuwa na jumla ya ndege nane, alisema mkurugenzi hiyo.

You can share this post!

Miguna Miguna arudishwe nchini, mahakama yaamuru

KCB, Equity na Co-operative zashushwa na Moody’s

adminleo