• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 3:25 PM
Familia 710,000 kunufaika na msaada wa serikali

Familia 710,000 kunufaika na msaada wa serikali

Na BERNARDINE MUTANU

FAMILIA kufikia 710,000 kote nchini zitapokea msaada kutoka kwa serikali mwishoni mwa Februari.

Fedha hizo ambazo hutolewa mara moja kila baada ya miezi miwili zitanufaisha watu wasiojiweza katika jamii.

Mradi huo, ‘Inua Jamii’ unalenga kupunguza viwango vya umaskini katika jamii. Pesa hizo ni za Novemba na Desemba 2017.

Watu hao watanufaika kutokana na ufadhili wa Sh2.8 bilioni na zitatolewa kupitia kwa afisi za kaunti ndogo na afisi za kaunti.

Chini ya mpango huo, serikali ilitoa Sh1.4 bilioni kwa watoto mayatima na maskini, Sh188 milioni kwa walemavu na Sh1.24 bilioni kwa wazee walio na miaka 65 na zaidi.

Awamu ya utoaji wa fedha hizo itakamilika Februari 22, alisema Katibu Mkuu katika Idara ya Kusimamia Maslahi ya Kijamii, Susan Mochache.

You can share this post!

Juhudi za Kenya kununua ndege za kijeshi zagonga mwamba

Bei ghali ya mafuta kupandisha gharama ya maisha

adminleo