Na WINNIE ATIENO
GAVANA wa Mombasa Hassan Joho ametetea azma yake ya kuwania urais akisema hana mzaha kuhusu suala hilo.
Bw Joho alisema Jumatano kuwa ingawa safari yake ya siasa ilianza kama mzaha, alitimiza malengo yake na kushangaza waliokuwa wakimpuuza.
“Nilipotangaza ninataka kuwa gavana, marafiki wangu walinicheka lakini nitashinda. Wanaopinga azma yangu ya urais wajue sina mzaha,” akasema.
Bw Joho alisema atapigania kuteuliwa na chama cha ODM kuwa mwaniaji wake wa urais mwaka ujao.
Bw Joho alikuwa akizungumza ofisini mwake jijini Mombasa alipompokea Mbunge Mwakilishi wa Kike wa Kaunti ya Nairobi, Bi Esther Passaris.
Aliwataka Wakenya kukumbuka ghasia za uchaguzi wa 2007 na kukoma kugawanywa, na badala yake waendelee kuishi kwa amani.
Kwa upande wake, Bi Passaris alimtaka Bw Joho kutangaza ramsi azma yake ya kuwania urais akiwa Nairobi.