• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Hatimaye Uhuru atangaza nafasi za makamishna IEBC

Hatimaye Uhuru atangaza nafasi za makamishna IEBC

Na BENSON MATHEKA

RAIS Uhuru Kenyatta hatimaye ametangaza nafasi nne za makamishna wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuwa wazi. Hatua hiyo imetoa nafasi ya kubuniwa kwa jopo la kujaza nafasi hizo.

Nafasi hizo zilibaki wazi kufuatia kujiuzulu kwa makamishna Roselyne Akombe, Consolata Maina, Margaret Mwachanya na Paul Kurgat.

Kulingana na sheria, Rais Kenyatta anapaswa kutangaza nafasi za makamishna zinazobaki wazi katika muda wa siku saba baada ya kupokea barua za kujiuzulu, lakini hakufanya hivyo.

Hii ina maana kuwa Rais Kenyatta alivunja sheria kwani imemchukua miaka mitatu kutangaza nafasi hizo kuwa wazi. IEBC imekuwa ikihudumu na makamishna watatu ambao ni pamoja na Bw Chebukati, Profesa Abdi Yakub Guliye na Bw Boya Molu.

Kumekuwa na miito ya kujazwa kwa nafasi hizo kutoka kwa wanasiasa lakini hilo halingewezekana bila rais kuzitangaza kuwa wazi au kuvunjwa kwa tume hiyo.

Bw Chebukati amewahi kulaumu bunge kwa kutoweka sheria za kufanikisha kujazwa kwa nafasi za makamishna wa tume.Mwaka jana, Bi Maina aliteuliwa naibu balozi nchini Italia sawa na Bi Mwachanya aliyetumwa Pakistan naye Bw Kurgat akatumwa Urusi.

You can share this post!

Tangatanga walia kuteswa na wandani wa Uhuru

Wakili Murgor akana vikali kuwa mkorofi