• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 3:25 PM
Johana na timu yake ya Jonkopings waangukia pua ligini Wambani akiokoa Vasalunds Uswidi

Johana na timu yake ya Jonkopings waangukia pua ligini Wambani akiokoa Vasalunds Uswidi

Na GEOFFREY ANENE

Jonkopings Sodra anayochezea Mkenya Erick Johana Omondi imetupwa kutoka juu ya jedwali ya Ligi ya Daraja ya Pili Uswidi hadi nambari sita.

Hii ni baada ya kuchabangwa na wenyeji Norrby 2-0 Jumatatu.

Mabao ya Norrby yalifungwa na Bubacarr Jobe na Nicklas Savolainen mapema katika kila kipindi. Ulikuwa ushindi wa kwanza wa Norrby dhidi ya Jonkopings nyumbani na pia katika mechi tatu.

Vasalunds anayochezea beki Mkenya Anthony Wambani ilisalia bila ushindi katika mechi zake mbili za kwanza baada ya kutoka sare ta 2-2 dhidi ya wageni Trelleborgs. Mai Traore aliweka Vasalunds kifua mbele dakika ya 55, lakini timu hiyo ikajipata chini 2-1 baada ya Abdul Safiu Fatawu na Johan Blomberg kufunga dakika ya 62 na 70, mtawalia.

Wambani aliokoa timu yake kupoteza mchuano wa pili mfululizo aliposawazisha 2-2 dakika ya 73. Bao la Wambani lilikuwa lake la kwanza katika mechi 10.

Jonkopings ni ya sita kwa alama tatu nayo Vasalunds inapatikana katika nafasi ya 15 kwa alama moja kwenye ligi hiyo ya klabu 16.

Timu ya Jonkopings itaalika nambari 10 Helsingborg mnamo Aprili 27 nayo Vasalunds izuru nambari 13 Vasteras mnamo Aprili 26 katika mechi zao zijazo. GAIS iko kileleni kwa alama sita.

  • Tags

You can share this post!

Leeds United wanyima Liverpool fursa ya kutinga ndani ya...

SHINA LA UHAI: Dhiki ya wagonjwa huku vikwazo vya Covid...