NA ASSUMPTA WAUSI
Niketipo nina haya ,yanisakama maizi
Kaozwa pasi na haya ,mtoto bila ujuzi
Ilikuwa ja ruiya ,kakatiziwa ulezi
Mtima una kilio,huku kazi kazi kazi .
Mi mtoto kama yaya ,watoto ninao zizi
Niko nyumbani kuleya ,nguvu ninazo tukizi
Nipitiayo hekaya ,kapatwa nayo machozi
Mtima una kilio ,huku kazi kazi kazi .
Nionapo wa ulaya ,wenzangu wana mizizi
Wako na bashasha ghaya ,mwenzenu kwa usingizi
Elimu yao kamwaya ,mwangaza si kama juzi
Mtima una kilio ,huku kazi kazi kazi .
Bukrata wa ashiya ,mbuzi ,ng’ombe zote hizi
Msimu wa gonjwa baya, baridi sina malazi
Kuozwa kweli kinaya ,mapema kama ndizi
Mtima una kilio ,huku kazi kazi kazi.
#GirlChildVoice