• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
Sababu za Ruto kutia miamba 5 tumbojoto

Sababu za Ruto kutia miamba 5 tumbojoto

Na WANDERI KAMAU

UJASIRI mkubwa alio nao Naibu Rais William Ruto kwamba atamrithi Rais Uhuru Kenyatta, licha ya vizingiti vilivyoko mbele yake, ni miongoni mwa sababu kuu zinazomfanya kuogopwa na vigogo wengine wa siasa nchini.

Kufikia sasa, Dkt Ruto hajaelezea nia yoyote ya kubuni muungano wa kisiasa na vigogo wengine.

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio wiki iliyopita, Dkt Ruto alisema “hataunda miungano ya kikabila” akisisitiza huo si mkakati wa mrengo wake wa ‘Hustler Nation.’

Hata hivyo, wadadisi wa siasa wanasema tatizo kuu linalomwandama Dkt Ruto ni ahadi aliyotoa Rais Kenyatta kwamba, atamuunga mkono kuwa mrithi wake kwa miaka kumi atakapomaliza kipindi chake 2022.

Mnamo 2016, Rais Kenyatta alisema baada ya kumaliza kuhudumu kwa miaka kumi, angemuunga mkono Dkt Ruto kuiongoza nchi kwa miaka 10 pia.

“Dkt Ruto anaonekana kushikilia kuwa lazima Rais Kenyatta atimize ahadi yake kama alivyosema. Anaamini Rais anastahili ‘kumrudishia mkono’ kwa kumfanyia kampeni mnamo 2013 na 2017,” asema mdadisi wa siasa Mark Bichachi.

Anasema imani hiyo ndiyo imemfanya kuunda kundi la ‘Tangatanga’, lengo kuu likiwa kuonyesha ana uwezo wa kujitafutia wafuasi bila uungwaji mkono wa Rais.

“Anaporejelea kuwa mrengo wake una wananchi na Mungu, ni ishara ya kupoteza imani kabisa kupata uungwaji mkono wa serikali, kinyume na ilivyokuwa kabla ya uhusiano wao na Rais Kenyatta kudorora. Ni msimamo huu ambao pia unaakisi masaibu ambayo baadhi ya washirika wake wa kisiasa wamekuwa wakipitia,” asema Bw Bichachi.

Wadadisi wanasema sababu nyingine ya Dkt Ruto kuogopwa na vigogo wengine wa kisiasa ni kwa sababu anawachukulia kama wasaliti.

You can share this post!

Ruto atawezana?

Malengo yangu ni kushindia PSG taji la kwanza la UEFA...