• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
STEPHEN JACKSON: Mifumo thabiti ya lishe kufaa uchumi na kukabiliana na njaa

STEPHEN JACKSON: Mifumo thabiti ya lishe kufaa uchumi na kukabiliana na njaa

Na Dkt STEPHEN JACKSON

NI mara chache ambapo sisi hufikiria kuhusu kinachohitajika ili chakula tunachokula kifike kwenye sahani zetu.

Kutoka “shambani hadi mezani,” wengi wetu hawatambui orodha kamili ya wahusika na michakato inayohusika.

Mfumo wa chakula unajumuisha wahusika wengi katika hatua mbalimbali za usafirishaji, utengenezaji, usambazaji, uhifadhi, na uuzalishaji.

Mifumo hii ikifanyika vizuri, italeta ustawi kiuchumi. Sekta ya kilimo nchini Kenya inayouza bidhaa nje ya nchi huajiri takriban robo tatu ya wafanyakazi na huzalisha robo moja ya Jumla ya Pato la Nchi (GDP) la kila mwaka.

Hata hivyo, Janga la Tabianchi la Ulimwengu lina maana kwamba kaunti nyingi za Kenya huteseka kutokana na ukame unaotokea mara kwa mara na kuongezeka kwa viwango vya upungufu wa lishe.

Matokeo yake ni upungufu wa maji, upungufu mbaya wa mimea, utapiamlo kwa watoto, upungufu wa malisho ya mifugo unaosababisha mifugo kutoa maziwa machache, hivyo basi kupunguza hali ya lishe.

Kufikia sasa, kaunti 12 kati ya 23 zilizo katika sehemu kame zimepokea tahadhari ya kukumbwa na ukame.Ulimwenguni, dunia yetu inazalisha na kutumia kiasi kikubwa cha chakula.

Lakini watu milioni 700 bado wanaathiriwa na njaa.

Teknolojia ya uzalishaji chakula imepevuka sana, lakini bado tunapambana na kiwango kikubwa kisichoweza kudumishwa cha uzalishaji wa gesi chafu zinazotoka kwenye viwanda na magari.

Hasara baada ya mavuno, hasa, ni changamoto kubwa nchini Kenya na kwingineko. Mambo mengine yanayovuruga mfumo wa chakula yanajumuisha mashambulizi kwa mabadiliko ya tabianchi, kutolingana kunakowazuia watu kufikia chakula wanachohitaji, na tatizo la uhifadhi.

Hivyo basi, kushughulikia vizuri Mifumo ya Chakula ni jambo la lazima ili kuwe na Maendeleo Endelevu. Ndiposa Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Antònio Guterres ameitisha “Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Mifumo ya Chakula” wa ulimwengu mzima tarehe 23 Septemba 2021.

Serikali, mashirika ya kiraia, sekta binafsi na watu ulimwenguni kote, watakusanyika kujadili namna ya kushirikisha mifumo ya chakula ili kuleta suluhisho kwa changamoto za ulimwengu za njaa, janga la tabianchi, umaskini, na kutokuwepo kwa usawa.

Mkutano huo wa wakuu wa nchi utatoa nafasi, si tu kwa viongozi ulimwenguni bali pia kwa wakulima, wajasiriamali, wanaharakati, na kila mtu anayehusika katika mchakato wa chakula ili kubadili jinsi ulimwengu unazalisha, unatumia na unafikiria kuhusu chakula.

Serikali ya Kenya imejitolea kugeuza mifumo yake ya chakula.

Kujitolea huku ni wazi kutokana na ruwaza ya 2030 na “Ajenda Kuu Nne” (Yanayofanya Dhamana ya Chakula na Lishe kwa Wakenya wote kuwa kipaumbele kwa taifa).

Mkakati wa Sekta ya Kilimo ya Kenya wa Ugeuzi na Ustawi unaonyesha kujitolea kwa serikali ya Kenya kuzidisha uzalishaji, kuinua mapato katika viwanda vya huduma za kilimo na kuhakikisha uthabiti wa makazi na dhamana ya chakula, kuwafanya wakulima wawe wadau wakuu ili kutimiza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Mkutano

Tunapoelekea kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Samaki na Mashirika pamoja na UN Kenya walikuwa na msururu wa mazungumzo ya kimaeneo, ya Taifa na Kitaifa ili kuwapa Wakenya nafasi ya kuchangia moja kwa moja kwa maono na malengo yanayonuia makuu ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi.

Mazungumzo hayo yameleta pamoja wadau wengi. Kwa makusudi, sauti zinazosikika mara chache zilijumuishwa na kutoa nafasi muhimu kwa washiriki kujadiliana, kushirikiana, na kupanga matendo ya kuwa na siku za usoni zilizo bora zaidi.

UN Kenya itaendelea kuisaidia serikali kwa kipindi kifupi na kirefu kuhakikisha mifumo ya chakula imeimarishwa na kusimamiwa ifaavyo.

Tunawasaidia wakulima wenye mashamba madogo kwa kuwapa mikopo na kuendeleza uwezo wao wa kufikia masoko.

Sisi hutoa usaidizi wa kutuma fedha kwa watu walio wepesi kudhurika katika mchakato wa usambazaji – hasa wakimbizi na jamii ambazo ni wenyeji wao.

Kuhusu kukabili ukame na kupunguza janga la tabianchi, UN Kenya inasaidia katika uzalishaji wa mbegu mbalimbali zinazochukua muda mfupi kukomaa na zinazostahimili ukame.

Hii inawasaidia wakulima kukuza mimea hata wakati wa ukame.

Aidha, kwa pamoja na washirikawenza, tunasaidia serikali za kaunti kukarabati au kujenga mabwawa mapya ya maji, tukiwasaidia wakulima kuongeza idadi ya mifugo yao na kukuza miradi ya fanya kazi-pata pesa.

Dkt. Stephen Jackson ni Mratibu Mkazi katika nchi ya Kenya 

You can share this post!

FKF yampa kocha mpya miezi 2 tu

WARUI: Tukumbatie changamoto za CBC ili utekelezaji uwe...