• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Avunja vyombo nyumbani kujua vilitoka kwa kimada wa mumewe

Avunja vyombo nyumbani kujua vilitoka kwa kimada wa mumewe

NA NICHOLAS CHERUIYOT

CHEBUNYO, CHEPALUNGU

MWANADADA mwenye hasira alivunjavunja vyombo vya jikoni alivyoletewa na mumewe baada ya kujua vilitoka kwa kimada wa mumewe.

Kwa mujibu wa mdokezi wetu, mke huyo alishangaa mumewe kumletea vyombo akidai amekuwa akivitumia kupika mjini anakofanya kazi.

Demu hakuamini kwani mumewe hapendi kupika na akaamua kuchunguza jambo hilo kisiri.

Alifanikiwa kupekua simu ya mzee na kubaini kuwa alivitwaa kutoka kwa kimada baada ya kukosana naye.

“Moja kwa moja alitoa nje vyombo hivyo na kuvipasua kwa nyundo na kuvikanyaga huku akilaani hatua ya mumewe. Jombi alipojua amepatikana alitoka nje ya boma kuhepa kioja kisha akarudi baadaye kuomba msamaha,” mdaku akaarifu.

  • Tags

You can share this post!

COP28: Kenya kupokea kima cha Sh1.5 bilioni kuangazia...

NSC yatahadharisha Wakenya kuhusu aina 30 za uhalifu msimu...

T L