NA TITUS OMINDE
MSHUKIWA aliyepatikana akikuza bangi katika mtaa wa Elgon-View mjini Eldoret Ijumaa alikamatwa baada ya kujisalimisha kwa polisi.
Michael Kibet Kipchumba alikiri kwa polisi kuwa anamiliki nyumba ambako polisi walipata bangi ikikuzwa.
Alizuiliwa kwa siku tatu. Kesi hiyo itatajwa Julai 12.