• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 6:50 AM
Ashtakiwa kwa kuiba taa ya gari katika kituo cha polisi

Ashtakiwa kwa kuiba taa ya gari katika kituo cha polisi

NA RICHARD MUNGUTI

MWANAMUME aliyefumaniwa akiiba vipuri vya gari la Serikali lililoegeshwa katika kituo cha polisi cha Kilimani ameshtakiwa.

James Mutua Kitheka mwenye umri wa miaka 53 alikiri mbele ya hakimu mkazi Jacqueline Ojwang kwamba alikamatwa akiiba ndani ya kituo cha polisi.

Mutua alikuwa ameiba taa ya gari aina ya Prado ya thamani ya Sh40,000.

Mahakama ilielezwa Mutua alionekana akitembea katika egesho la magari katika kituo hicho cha polisi.

Alionekana akifungua gari hilo na kuanza kupora vipuri.

Alikiri alitekeleza wizi huo mnamo Juni 8, 2022.

Mshtakiwa alikamatwa kwa kuiba vipuri kutoka kwa gari hilo la GK lililokuwa limeegeshwa nje ya afisi za idara ya trafiki kituoni hapo.

Mahakama iliombwa isimhukumu mshtakiwa ili polisi walete taa iliyoibwa.

  • Tags

You can share this post!

Wapishi ndani kwa wizi wa chakula cha shule

Sonko anahatarisha kura Mombasa – IEBC

T L