• Nairobi
  • Last Updated May 9th, 2024 11:34 AM
Brazil kumalizana na Colombia leo usiku

Brazil kumalizana na Colombia leo usiku

RIO DE JANEIRO, Brazil

Huku mechi za makundi za kuwania ubingwa wa Copa America zikendelea, Brazil na Colombia zimepangiwa kukutana katika Kundi la B jijini hapa, leo usiku.

Ni mechi inayotarajiwa kuwa ngumu kwa pande zote ikikumbukwa kwamba timu hizo ndizo zinazomiliki nafasi za juu kwenye kundi hilo.Brazil wanaongoza baada ya kushinda mechi mbili za kwanza, wakati Colombia wakikamata nafasi ya pili.

Mabingwa hao wa zamani ni miongoni mwa timu zinazowekewa matrumaini makubwa ya kutwaa ubingwa baada ya kushinda taji hilo mnamo 2019 kwa mara ya mwisho.

Walianza kampeni zao kwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Venzuela kutokana na mabao ya Marquinhos, neymar na Gabriel Barbosa.Baadaye vijana hao wa kocha Tite waliandikisha ushindi mwingine mkubwa wa 4-1 dhidi ya Peru.

Wafungaji katika mechi hiyo walikuwa Alex Sandro, Ribeiro na Richardarlison aliyepachika wavuni mawili mechi ikielekea kumalizika.Kutokana na matokeo hayo ya kuridhisha, Brazili wanawekewa matumaini ya kuendelea kung’ara katika mashindano haya yaliyohamishwa hadi Brazil kutokana na maambukizi ya virusi nchini Argentina.

Hata hivyo, huenda wakakumbwa na kazi ngumu mbele ya Colombia wanaoelewa umuhimu wa mechi hii yao ya mwisho kundini. Vijana hao wa kocha Reinaldo Rueda wamefanikiwa kupata pointi nne kutokana na mechi tatu, baada ya ushindi pekee wa 1-0 dhidi ya Ecuador mjini Cuiaba.

Walianza kwa sare ya kutofungana dhidi ya Venezuela, kabla ya kuchapwa 2-1 na Peru, ambayo ilikuwa imelimwa 4-0 nba Brazil katika mechi ya awali.Katika mechi nyingine ya kundi la B, Ecuador imepangiwa kucheza na Peru kuanzia usiku wa manane.

  • Tags

You can share this post!

Pesa za wazee ziwafae wajane

Wajerumani walikosa kuongeza idadi 2020