• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
Jinsi vijana wanne walivyouawa Buruburu kwa kumiminiwa risasi  

Jinsi vijana wanne walivyouawa Buruburu kwa kumiminiwa risasi  

NA MWANGI MUIRURI 

RIPOTI ya upasuaji wa miili ya vijana watatu kati ya wanne waliouawa Jumapili, Desemba 24, 2023, mtaani Buruburu, Nairobi imebaini kuwa walifariki kutokana na kufuja damu kupita kiasi kufuatia majeraha ya risasi.

Mmoja wa waathiriwa hao, Brian Mwangi Kariuki wa umri wa miaka 24 aliuawa kwa kupigwa risasi 12 mwilini na ni moja tu ambayo ilipatikana kwenye paja la mguu, hizo nyingine zote zikiwa zilimwingia na zikatoka.

Naye kijana Julius Mwangi, 25, alikuwa na risasi sita mwilini, huku Benson Mwangi Kinyua, 22, akipatikana na majeraha ya risasi tano, zote zikiingia na kutoka.

Mwili wa nne bado haujafahamika na ulikuwa na risasi nane mwilini.

Vijana hao walikumbana na maafa wakiwa kwenye gari walilokuwa wakiendesha.

Upasuaji huo ulifanywa na Dkt Peter Ndegwa.

Mtaalamu huyo alisema kwamba vijana hao walilengwa kwa karibu na wahuni waliowaangamiza.

[email protected]

  • Tags

You can share this post!

Mmoja wa waliouawa Buruburu alikuwa mchuuzi wa nguo na viatu

Krismasi: Alivyorambwa kwenye baa akijigamba mbele ya...

T L