NA SAMMY WAWERU
BINAMUYE muimbaji hodari wa nyimbo za Mugithi Samuel Muchoki, Bernice Saroni amemsuta seneta maalum Karen Nyamu kwa kunyakua mume wa wenyewe.
Bw Muchoki maarufu kama Samidoh, ni mume wa Edday Nderitu na wanandoa hao wana watoto watatu.
Kulingana na Bernice, changamoto kuu kuwa kwenye uhusiano haramu na mume wa mwingine ni ushindani unaojiri.
Kwake binamu wa Samidoh ni suala ambalo kamwe hawezi kulikaribisha moyoni, kwani ana ‘wivu wa mapenzi’.
“Jambo baya zaidi kuwa na uhusianon kimapenzi na mwanamume aliyeoa, utakuwa kwenye dunia ya ushindani,” Bernice aliandika kupitia chapisho la Facebook, katika akaunti yake rasmi.
“Kisha wivu weeeh…Hilo sitaweza,” alielezea.
Chapisho hilo linafasiriwa kuwa ujumbe kwa Karen Nyamu, ambaye ni seneta maalum wa chama cha UDA.
Kulingana na maelezo binafsi ya Bernice Facebook, ni Mtaalamu wa Masuala ya Kiakili Massachusetts, Amerika.
Mwanadada huyo, mwishoni mwa mwaka uliopita alisitiri Samidoh kwa kumpa mahali pa kulala kufuatia mwaliko wake ng’ambo kutumbuiza mashabiki wake wa Mugithi.
Aghalabu, walikuwa wanapiga picha katika kila ziara, Bernice akipakia kwenye akaunti yake ya Facebook.
Kabla kurejea nchini, Karen Nyamu alizua drama katika eneo moja la burudani Dubai alikokuwa akitumbuiza mashabiki.
Nusra Karen na mke wa kwanza wa Samidoh watwangane.
Samidoh na Karen wamepata watoto wawili pamoja.