• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 3:16 PM
Karen Nyamu ‘ashambuliwa’ na binamuye Samidoh

Karen Nyamu ‘ashambuliwa’ na binamuye Samidoh

NA SAMMY WAWERU

BINAMUYE muimbaji hodari wa nyimbo za Mugithi Samuel Muchoki, Bernice Saroni amemsuta seneta maalum Karen Nyamu kwa kunyakua mume wa wenyewe.

Bw Muchoki maarufu kama Samidoh, ni mume wa Edday Nderitu na wanandoa hao wana watoto watatu.

Kulingana na Bernice, changamoto kuu kuwa kwenye uhusiano haramu na mume wa mwingine ni ushindani unaojiri.

Kwake binamu wa Samidoh ni suala ambalo kamwe hawezi kulikaribisha moyoni, kwani ana ‘wivu wa mapenzi’.

“Jambo baya zaidi kuwa na uhusianon kimapenzi na mwanamume aliyeoa, utakuwa kwenye dunia ya ushindani,” Bernice aliandika kupitia chapisho la Facebook, katika akaunti yake rasmi.

“Kisha wivu weeeh…Hilo sitaweza,” alielezea.

Chapisho hilo linafasiriwa kuwa ujumbe kwa Karen Nyamu, ambaye ni seneta maalum wa chama cha UDA.

Seneta maalum Karen Nyamu. PICHA / MAKTBA

Kulingana na maelezo binafsi ya Bernice Facebook, ni Mtaalamu wa Masuala ya Kiakili Massachusetts, Amerika.

Mwanadada huyo, mwishoni mwa mwaka uliopita alisitiri Samidoh kwa kumpa mahali pa kulala kufuatia mwaliko wake ng’ambo kutumbuiza mashabiki wake wa Mugithi.

Aghalabu, walikuwa wanapiga picha katika kila ziara, Bernice akipakia kwenye akaunti yake ya Facebook.

Muimbaji wa Mugithi Samuel Muchoki almaarufu Samidoh na binamu yake Bernice Saroni. PICHA / HISANI

Kabla kurejea nchini, Karen Nyamu alizua drama katika eneo moja la burudani Dubai alikokuwa akitumbuiza mashabiki.

Nusra Karen na mke wa kwanza wa Samidoh watwangane.

Samidoh na Karen wamepata watoto wawili pamoja.

  • Tags

You can share this post!

Uteuzi mwenyekiti IEBC, makamishna sita kuendelea

Mombasa yatuzwa kwa huduma bora za afya nchini

T L