• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Karo: Magoha ataka watoto wafukuzwe

Karo: Magoha ataka watoto wafukuzwe

DAVID MUCHUNGUH na SIMON CIURI

WAZIRI wa Elimu, Prof George Magoha, jana aliwapa maagizo walimu wakuu kuwafukuza wanafunzi ambao wana madeni ya karo, baada ya malalamishi kutoka kwa walimu hao kuwa hawana fedha za kuendeshea shule.

Hilo linamaanisha huenda leo wanafunzi wakafukuzwa kutoka shuleni, siku moja tu baada yao kurejea kutoka mapumziko ya kati ya muhula.Kinyume na msimamo wake wa awali, Prof Magoha aliwalaumu wazazi kwa kutotekeleza majukumu yao kama wanavyohitajika.

Imekuwa kawaida kwa waziri kuwatetea wanafunzi dhidi ya kufukuzwa shuleni kutokana na matatizo ya kutolipa karo.“Idadi kubwa ya watu ambao hawalipi karo wana uwezo wa kifedha. Licha ya agizo hilo, nawarai walimu wakuu kuhakikisha wanafunzi wanowafukuza hawatoki katika familia maskini au mlezi wa mwanafunzi husika amepoteza ajira.’

Watu wengi wanatoa visingizio vya athari za janga la virusi vya corona. Kwa sasa, nawapa uhuru kuchukua hatua kuhakikisha karo zinalipwa,” akasema Prof Magoha.Alitoa kauli hiyo jana kwenye hafla ya kufungua maabara maalum ya kilimo iliyojengwa na serikali ya Japan katika Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT), eneo la Juja, Kaunti ya Kiambu.

Wiki iliyopita, walimu wakuu walilalamika kuwa shughuli nyingi muhimu zimekwama kutokana na wazazi kutolipa karo.Walisema shule nyingi zinadaiwa mamilioni ya fedha na watu ambao hutoa huduma muhimu kwa shule.“Lazima wazazi wawajibikie majukumu yao ifaavyo kwa kulipa madeni ya karo iliyobaki.

Hili litaziwezesha shule kuepuka baadhi ya changamoto za kifedha zinazoziandama kwa sasa,” akasema Bw Kahi Indimuli, ambaye ndiye mwenyekiti wa Chama cha Kitaifa cha Walimu wa Shule za Upili (KESSHA).Awali, shule zilikuwa zikishikilia vyeti vya wanafunzi hadi walipe karo yote.

pale walipomaliza kulipa madeni ya karo waliyodaiwa.Hata hivyo, serikali iliziagiza shule kutoshikilia vyeti vya wanafunzi hata ikiwa wanadaiwa madeni ya karo.

You can share this post!

Mvutano wa kuvunja serikali ya Vihiga waendelea

Achani arai wanawake wajitokeze zaidi kisiasa