NA BENSON MATHEKA
RAIS William Ruto jana Jumanne alimsamehe aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Matibabu Kenya (KEMRI), Dkt Davy Koech ambaye alikuwa akitumikia kifungo cha miaka sita jela kwa ufisadi wa Sh19.3 milioni.
Dkt Koech alikuwa kati ya watu 37 na wafungwa zaidi ya 2,900 wa makosa madogo ambao Rais Ruto alisamehe kabla ya kukamilisha kifungo chao.