• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
Liverpool kurudiana na RB Leipzig kwenye hatua ya 16-bora UEFA jijini Budapest, Hungary

Liverpool kurudiana na RB Leipzig kwenye hatua ya 16-bora UEFA jijini Budapest, Hungary

Na MASHIRIKA

LIVERPOOL watacheza mechi yao ya nyumbani kwenye marudiano ya hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu huu dhidi ya RB Leipzig ya Ujerumani uwanjani Puskas Arena, Budapest, Hungary.

Mchuano huo umehamishwa hadi jiji hilo kuu la Hungary kwa sababu ya ukali wa masharti ya kudhibiti msambao wa virusi vya corona.

Liverpool ya kocha Jurgen Klopp itajibwaga ugani kwa minajili ya mechi hiyo ikijivunia ushindi wa mabao 2-0 kutokana na mchuano wa mkondo wa kwanza uliochezewa katika uwanja uo huo wa Puskas Arena mnamo Februari 16, 2021.

Mechi hiyo ya mkondo wa pili imeratibiwa kutandazwa mnamo Jumatano ya Machi 10, 2021.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Simba wa Ford Kenya anguruma Kabuchai

Bilbao kucheza fainali mbili za Copa del Rey mnamo Aprili...