• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 5:20 PM
Mabadiliko yafanyika katika ngazi za utawala maeneo kadha Nairobi

Mabadiliko yafanyika katika ngazi za utawala maeneo kadha Nairobi

Na SAMMY KIMATU

MABADILIKO ya maafisa wa utawala yamefanyika katika maeneo tofauti tofauti katika kaunti ya Nairobi.

Katika tarafa ya South B, Msaidizi wa kamishna wa kaunti Bw Michael Aswani Were alisema miongoni mwa maafisa ni pamoja na waliopanda ngazi huku wengine wakihamishwa.

Chifu Mkuu wa eneo la Landi Mawe ni Bw Solomon Muranguri ambaye alihudumu katika lokesheni ya Ngando, Kawangware katika kaunti ndogo ya Dagoretti.

Aliyekuwa chifu wa Landi Mawe kabla ya ujio wa Bw Muranguri, Bw Mulandi Kikuvi ndiye chifu mkuu wa eneo la Ngando.

Vile vile, Bw Charles Karanja aliyehudumu katika daraja la naibu chifu katika lokesheni ndogo ya Landi Mawe alipandishwa cheo na kuwa chifu.

Bw Karanja alihamia katika eneo la Golf Course lililoko katika kaunti ndogo ya Kibra.

Zaidi ya hayo, ni kwamba Bw Muranguri aliwahi kuhudumu katika lokesheni ya Landi Mawe kabla ya kubadilishwa na Bw Patrick Were aliyehamia Kabiria, Waithaka katika kaunti ndogo ya Dagoretti.

“Mabadiliko hayo yanahusisha zaidi maafisa ambao wamepata elimu ya juu wangali wakiwa kazini japo afisa wa serikali anaweza kuhudumu kote nchini,” Bw Were akasema.

  • Tags

You can share this post!

Amref yamtaka Uhuru aondoe kafyu

Kioja mama akiuza shamba aponde raha