• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 12:38 PM
Machifu sasa kulipwa pesa za kuinua motisha

Machifu sasa kulipwa pesa za kuinua motisha

Na CECIL ODONGO

MAAFISA wa utawala wamevuna marupurupu makubwa baada ya Tume ya Uajiri wa Watumishi wa Umma (PSC) kuidhinisha walipwe pesa za kuwatia motisha.

Katibu katika Wizara ya Usalama wa Ndani, Dkt Karanja Kibicho, alisema marupurupu hayo yatatolewa kuanzia kwa manaibu chifu hadi makamishna wa maeneo kullingana na wajibu wao na pia changamoto wanazopitia kazini.

Uamuzi wa kuwapa maafisa hao w pesa hizo uliafikiwa baada ya mkutano kati ya wizara hiyo na wanachama wa PSC.

Kabla ya kukubali malipo hayo mapya, PSC na SRC zilizingatia majukumu ya ziada ya kila afisa, usawa, aina ya kazi yao na gharama ya kuyatekeleza bila gharama kubwa.

You can share this post!

DOMO KAYA: Mtakuja kupigwa kiboko!

Kenya yachukua ubingwa katika soko la mihadarati