• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 3:16 PM
Magaidi wa Al-Shabaab wazidiwa nguvu na walinzi wa Kenya katika shambulio kambini

Magaidi wa Al-Shabaab wazidiwa nguvu na walinzi wa Kenya katika shambulio kambini

NA KALUME KAZUNGU

MAAFISA wa usalama katika Kaunti ya Lamu, jana walitibua jaribio jingine la mashambulio katika kambi ya wakimbizi iliyoko Shule ya Msingi ya Juhudi, ambayo iliwahi kuvamiwa pia Julai.

Naibu Kamishna wa Lamu Magharibi, Bw Gabriel Kioni, alithibitisha kuwa kundi la magaidi waliokuwa na bunduki walivamia kambi hiyo majira ya saa tisa unusu usiku wa kuamkia jana.

Walianza kufyatua risasi kila upande lakini wakatimuliwa na maafisa wa usalama waliowashinda nguvu ikawabidi kutorokea msituni Boni.

Shambulio hilo lilitokea siku mbili pekee baada ya watu wawili kuuawa katika eneo la Lango La Simba kwenye barabara kuu ya Lamu-Witu-Garsen.

  • Tags

You can share this post!

Sumu hatari zimeachiliwa ndani ya Mto Athi, bunge laelezwa

Lukaku: Ilibidi tuzoee maziwa na mkate kila siku kwa sababu...

T L